Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Madhara ya dawa za kulevya kwa mwili na ubongo

Featured Image
Moja kati ya vitu vinavyotisha kuhusu dawa za kulevya ni kwamba zinaathiri watu kwa njia mbalimbali na huwezi ukasema kwa uhakika jinsi zitakavyokuathiri. Madhara ya dawa za kulevya yanategemea aina, kiwango na jinsi zitakavyotumika. Vilevile inategemea na umri, afya ya mwili na ukomavu wa akili, na pia mazoea ya matumizi ya dawa hizo. Madhara ya muda hutokea mara tu baada ya dawa za kulevya kutumika, wakati madhara ya muda mrefu huonekana baada ya muda kupita, na mara nyingi husababisha uharibifu wa kudumu kwenye mapafu na ubongo. Kwa mfano, bangi, husababisha kuongezeka kwa mapigo ya moyo, matatizo ya kumbukumbu ya muda mfupi, pamoja na umakini, kujifunza, kufikiri na kutatua matatizo. Pia inaweza ikasababisha kasoro kwenye utaratibu wa viungo vya mwili. Mara kwa mara wavuta bangi huwa na macho mekundu. Na vijana wengine hupata mihemuko mbalimbali kama uoga na hofu baada ya matumizi ya bangi. Dawa za kulevya za vichangamsho, kama mirungi na kokaini, inasemekana kuwa huwafanya watumiaji kuwa macho, kujiona wana nguvu na kujiamini. Vichangamsho vikitumika kwa wingi, humfanya mtumaji kujihisi kuwa na wasiwasi au hofu. Matumizi mabaya ya dawa za kulevya kwa muda mrefu huweza kusababisha matatizo ya akili au hata kifo i iwapo yatatumika kwa kiwango cha juu. Dawa za kulevya zinazokufanya upooze kama heroini au dawa nyingine zinazoagizwa na daktari, husababisha kujisikia umetulia, una amani na furaha. Ukizidisha vipimo husababisha usingizi, upungufu wa umakini na uwezo wa kuona, kizunguzungu, kutapika na kutokwa jasho. Vilevile kipimo kingi kinaweza kusababisha usingizi wa muda mrefu, kuzimia na hata kifo. Pombe za kienyeji kama gongo ni hatari kwa afya na zinaweza kusababisha upofu na hata kifo. Matumizi ya dawa za kulevya hupunguza uwezo wa vijana kuhimili na kutatua matatizo yao ya kijamii na kiakili. Hii husababisha vijana kuwa wepesi kujihusisha na ujambazi na mambo ya ngono na ugomvi, mabadiliko hayo ya tabia husababisha ugomvi katika familia na kuvunjika kwa urafiki. Matumizi ya dawa za kulevya ndiyo sababu kubwa ya ajali za barabarani, kujiua na maambukizo mbalimbali.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuonyesha Ukarimu kwa Msichana Wako

Jinsi ya Kuonyesha Ukarimu kwa Msichana Wako

Habari za leo! Leo nataka kuzungumza juu ya jinsi ya kuonyesha ukarimu kwa msichana wako. Kama mw... Read More

Jinsi ya Kuvutia Wasichana: Vidokezo vya Kuchumbiana na Wasichana

Jinsi ya Kuvutia Wasichana: Vidokezo vya Kuchumbiana na Wasichana

Jambo rafiki yangu! Katika maisha ya kila siku, tunakutana na wasichana wengi ambao tunapenda kuw... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili matarajio ya ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, kuna umuhimu wa kujadili matarajio ya ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, kuna umuhimu wa kujadili matarajio ya ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano? Swali hili ni mo... Read More

Ubikira ni nini?

Ubikira ni nini?

Maana halisi ya neno โ€œbikiraโ€ ni mwanamke au mwanaume ambaye hajawahi kabisa kujamii ana. Kuj... Read More

Mapenzi salama ni yapi?

Mapenzi salama ni yapi?

Mapenzi salama ni yale yanayofanyika bila wasiwasi wa kupata mimba zisizotarajiwa, magonjwa ya zi... Read More

Kwa nini watu wanaamini kuwa Albino hawana maambukizo ya Virusi vya UKIMWI (VVU)?

Kwa nini watu wanaamini kuwa Albino hawana maambukizo ya Virusi vya UKIMWI (VVU)?

Imani hiyo si kweli kabisa. Inawezekana ni kupotoshwa kwa
makusudi wa ukweli kuhusu jambo hi... Read More

Je, ni kweli kwamba uvutaji wa bangi hupunguza mawazo?

Je, ni kweli kwamba uvutaji wa bangi hupunguza mawazo?

Bangi hupunguza mawazo kwa muda mfupi kwani huleta hisia za furaha na utulivu. Lakini hata hivyo ... Read More

Je, unyenyekevu una jukumu muhimu katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, unyenyekevu una jukumu muhimu katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, unyenyekevu una jukumu muhimu katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Kwa wengi, ngo... Read More

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kujaribu njia za kutanua wigo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mape... Read More

Je, mvulana afanye nini ili kuzuia ndoto nyevu?

Je, mvulana afanye nini ili kuzuia ndoto nyevu?

Ndoto nyevu ni kitu kinachowatokea vijana wakiwa usingizini. Haiwezekani kuzuiwa kwa sababu uko usin... Read More
Wakati wa makuzi/ kubalehe/ kuvunja ungo, ni mabadiliko gani yanatokea kwenye miili ya wasichana?

Wakati wa makuzi/ kubalehe/ kuvunja ungo, ni mabadiliko gani yanatokea kwenye miili ya wasichana?

Balehe ni kipindi cha mpito kati ya utoto na utu uzima, ambapo watoto wa ki... Read More

Je, nini imani ya watu katika kufanya mazoezi ya kujiongeza nguvu wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kufanya mazoezi ya kujiongeza nguvu wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Habari za leo rafiki yangu! Leo tutazungumzia jambo muhimu sana kwenye uhusiano wa mapenzi, ambal... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About