Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Mapishi ya Wali Wa Tambi Na Kuku Wa Sosi Ya Mtindi

Featured Image

Vipimo Vya Wali

Mchele - 3 vikombe

Tambi - 2 vikombe

Mafuta - ยผ kikombe

Chumvi

Vipimo Vya Kuku

Kuku kidari (boneless) aliyekatwa katwa vipande - 1 Kilo

Kitunguu maji kilichokatwa katwa - 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai

Chumvi - kiasi

Paprika - 1 kijiko cha supu

Masala ya kuku (tanduri au yoyote) - 1 kijiko cha supu

Ndimu - 2 vijiko vya supu

Mtindi (yoghurt) au malai (cream) - 1 kikombe

Mafuta - ยผ kikombe

Majani ya kotmiri (coriander) - ยฝ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali:

Osha Mchele, uroweke.
Tia mafuta katika sufuria, kaanga tambi zilizokatwakatwa hadi zigeuke rangi kuwa nyekundu.
Tia mchele endelea kukaanga kidogo.
Tia maji kiasi cha wali kupikika kama unavyopika pilau. Kiasi cha maji kinategemea aina ya mchele
Funika katika moto mdogo mdogo hadi uive ukiwa tayari.

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku

Katika bakuli, changanya vitu vyote isipokuwa mtindi na kitunguu.
Tia mafuta katika karai, kisha tia kitunguu ukaange muda mdogo tu, usikiache kugeuka rangi.
Tia kuku na masala yake, endelea kukaanga, kisha tia mtindi au malai ufunike apikike na kuiva vizuri.
Nyunyuzia kotmiri iliyokatwakatwa ikiwa tayari kuliwa na wali wa tambi.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Namna ya kutengeneza Visheti Vya Nazi Na Njugu (Sudani)

Namna ya kutengeneza Visheti Vya Nazi Na Njugu (Sudani)

VIAMBAUPISHI

Unga - 3 mug za chai

Samli - ยฝ mug ya chai

Maziwa - 1ยผ mug ya ... Read More

Mapishi ya Sponge keki

Mapishi ya Sponge keki

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour) 100g
Sukari (sugar) 100g
Siagi isiyok... Read More

Mawazo ya Chakula cha Usiku cha Dakika 20 kwa Familia Yote

Mawazo ya Chakula cha Usiku cha Dakika 20 kwa Familia Yote

Mawazo ya Chakula cha Usiku cha Dakika 20 kwa Familia Yote ๐ŸŒฎ๐Ÿ๐Ÿ—

Kama AckySHINE, le... Read More

Jinsi ya kupika mkate wa sembe

Jinsi ya kupika mkate wa sembe

Mahitaji:

Unga sembe glass 1
Unga ngano glass 1
Sukari glass 1 (unaweza kupungu... Read More

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Mahitaji

Mchele (rice vikombe 3)
Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo)
Viazi mbatata... Read More

Mapishi ya Samaki wa kupaka

Mapishi ya Samaki wa kupaka

Mahitaji

Samaki (Tilapia 2)
Nyanya ya kopo (Tomato tin 1)
Kitunguu (Onion 1)Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Samaki Na Mboga

Jinsi ya kupika Wali Wa Samaki Na Mboga

VIPIMO VYA SAMAKI

Samaki wa sea bass vipande - 1ย 1/2 LB (Ratili)
Kitunguu saumu(tho... Read More

Mapishi ya Bokoboko La Kuku

Mapishi ya Bokoboko La Kuku

Mahitaji

Ngano nzima (shayiri) - 3 Vikombe

Kuku - ยฝ (3 LB takriban)

Thomu na... Read More

Mapishi ya Bagia dengu

Mapishi ya Bagia dengu

Mahitaji

Unga wa dengu (gram flour 1/4 kilo)
Kitunguu kilichokatwa (onion 2)
Ho... Read More

Vyakula vya Kutayarishwa Mapema kwa Afya Vinavyofaa kwa Usiku wa Juma

Vyakula vya Kutayarishwa Mapema kwa Afya Vinavyofaa kwa Usiku wa Juma

Vyakula vya Kutayarishwa Mapema kwa Afya Vinavyofaa kwa Usiku wa Juma

๐ŸŒ™๐Ÿฅ˜

Usik... Read More

Mapishi ya Mchuzi wa kambale

Mapishi ya Mchuzi wa kambale

Mahitaji

Kambale 2
Nazi kopo 1
Nyanya kopo 1
Vitunguu 2
Curry powder ... Read More

Jinsi ya kupika Roast ya biringanya na mayai

Jinsi ya kupika Roast ya biringanya na mayai

Mara nyingi biringanya hutumika kama kiungo cha nyongeza katika mchuzi. Hata hivyo, kiungo hiki k... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About